Shirika la umeme nchini, TANESCO, limekuwa likipata hasara ya kati ya shilingi bilioni 109 na bilioni 189 kwa kila mwaka katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita kutokana na kuuza umeme kwa bei nafuu.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Nishati na Madini, Mhesmiwa William Ngeleja wakati akijibu swali la Mbunge wa Mlalo, CCM, Brigedia Jenerali (mstaafu) Hassan Ngwilizi.
Mheshimiwa Ngwilizi alitaka kujua kwanini bei za umeme zinazidi kupanda badala ya wananchi kufaidika na raslimali zilizopo nchini.
Akijibu swali hilo , Mhesimiwa Ngeleja akasema kuwa hasara hiyo ilipatikana katika kipindi cha kati ya mwaka 2004 na mwaka jana.
Akasema katika miaka ya nyuma, Serikali ilikuwa ikiipatia Tanesco ruzuku kwa ajili ya kufidia tofauti kati ya bei ya kuuzia umeme na gharama halisi za umeme nchini.
Hata hivyo, akasema kuanzia mwaka wa fedha wa 2007 na 2008, Serikali imesitisha utoaji wa ruzuku kwa shirika hilo na kuridhia kuwa bei za umeme ziwe zinarudisha gharama halisi za umeme.
Akafafanua kuwa inapaswa sasa shirika hilo lijiendeshe kibiashara na kuwa kutokana na hatua hiyo chanzo pekee cha mapato ya shirika hilo ni uuzaji wa umeme.
SOURCE: Alasiri, 22/4/2008
This blog contains information about what is happening in energy access development in Tanzania. You are welcome to give your thoughts and ideas on the issues published. Thank you.
Tuesday, April 22, 2008
TANESCO yapata hasara ya bilioni 189!
Posted by
Godfrey
at
21:39
0
maoni/comments
Saturday, April 05, 2008
Moto kuwaka bungeni keshokutwa hoja ya Richmond kuibuka upya
WIKI ijayo Waziri Mkuu, Mizengo Pinda anatarajiwa kupata mtihani wake wa kwanza bungeni atakaposimamia mapendekezo ya hatua zinazopaswa kuchukuliwa dhidi ya watu waliohusika katika kashfa ya Richmond.
Mtihani kwa Pinda unakuja kutokana na kuwapo taarifa kwamba suala hili la Richmond limewagawa wabunge katika sehemu mbili.
Wapo baadhi ya wabunge ambao wanadaiwa kuwa kambi moja na baadhi ya watu wanaotuhumiwa katika kashfa hiyo wakiendesha kampeni ya kuhakikisha suala hilo linakosa nguvu ya kujadiliwa katika kikao hicho na wengine wanaokwenda na mtazamo wa Watanzania.
Wabunge hawa pamoja na baadhi ya wana CCM wenye ushawishi mkubwa ndio ambao pia waliweka kambi Butiama wakati wa kikao cha Halmashauri Kuu (NEC) kuhakikisha kuwa hoja ya mafisadi kuchukuliwa hatua kichama inaizimwa.
Hata hivyo, wapo wabunge ambao wanapa na kuhakikisha kuwa suala la Richmond linajadiliwa na watu wote waliohusika na kashfa wanachukuliwa hatua bila upendeleo.
Joto la kashfa ya Richmond limezidi kuongezeka baada ya wiki hii bunge kutoa taarifa iliyokuwa ikituhumu kuwapo kwa kundi la watu nchini linaloeneza uvumi wa kutaka kumchafua Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano, Samuel Sitta.
Taarifa hiyo ya bunge ilikwenda mbali zaidi kwa kueleza kwamba njama hizo za kutaka kumchafua spika kumhusisha na ubadhirifu wa fedha za bunge zimekuja hivi sasa wakati bunge bado linashunglikia suala la Richmond.
Ni kutokana na hali hiyo ya mvutano mkubwa kuhusu Richmond, Waziri Mkuu Pinda atakuwa na mtihani kama kiongozi wa serikali bungeni kusimama kidete kuhakikisha kuwa ahadi yake ya kuona watu waliohusika na kashfa ya Richmond wanachukuliwa hatua zinazoshaili inafanyika.
Kama atakwama kusimamia serikali kuwachukulia hatua au timu aliyoiunda ambayo kwa mara ya kwanza ilimaliza kazi mapema kabla ya muda wake itakuja na mapendekezo hafifu ambayo haya maslahi kwa nchi, huenda ndiyo ikawa safari ya Pinda kuanza kuporomoka.
Wananchi bado wana imani na Pinda wanajua kwamba ni waziri mkuu mwenye msimamo ambaye husema kweli bila kuuma umma maneno yake.
Katika bunge lililopita aliapa kuwa wale wote watakaobainika kuhusika na kashfa hiyo bila ya kujali nyadhifa zao serikalini au ndani ya chama, watachukuliwa hatua za kisheria kama kawaida.
Hata hivyo, wachunguzi wa masuala ya kisiasa nchini wanaona Pinda ana kibarua kigumu kuwabana watu waliohusika katika kashfa hiy kutokana na ukweli kwamba ni watu wenye 'nguvu' hata ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) wana mizizi kiasi kwamba chama kinawagwaya.
Ukweli huu unadhihirishwa na kitendo cha CCM kushindwa kujadili hoja ya kuwachukulia hatua kichama watu wanachama ambao wanadaiwa kuchafuka kutokana na kuhusika katika kashfa za ufisadi.
Hata hivyo, Pinda naye ameanza kujitenga na mtihani huo, kwani hivi karibuni alikaririwa akisema kwamba baada ya kuipokea ripoti hiyo ataifanyia kazi na hatimaye kuiwasilisha kwa Rais Jakaya Kikwete kwa hatua na maelekezo yake.
Ripoti ya tume hiyo inafuatia taarifa ya Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza mchakato wa Zabuni ya Kampuni ya Richmond ya Houston, Texas Marekani ambapo Wabunge hao walijadili taarifa hiyo na kutoa jumla ya mapendekezo 23 ambayo serikali iliahidi kuyafanyia kazi.
Timu hiyo ya Pinda inahusisha wawakilishi kutoka Ikulu, sekretarieti ya mawaziri,Tume ya maadili, TAMISEMI, Wakala wa Manunuzi (PPRA), Makandarasi, Utumishi wa Umma na Mipango, itapitia mapendekezo hayo na kutoa dira ya namna ya kuyatekeleza.
Tume hiyo iliundwa kufuatia mapendekezo ya Kamati ya Bunge Iliyoongozwa na Dk Harrison Mwakyembe kutoa mapendekezo ya hatua zinazopaswa kuchukuliwa na serikali kwa waliohusika na kashfa ya Richmond.
Alitaja baadhi ya mapendekezo hayo kuwa Msajili wa Ofisi ya BRELA kuifuta Kampuni ya Richmond na wamiliki wake wote kufunguliwa kesi ya jinai, kisha serikali kuangalia uwezekano wa kusitisha malipo kwa kampuni ya Dowans.
Alisema serikali pia ilitakiwa kuendesha uchunguzi wa kina kubaini taarifa tete kuwa taarifa ya Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru) kuhusu Richmond ilichezewa na kuitafuta taarifa halisi ya taasisi hiyo.
Mapendekezo mengine ni serikali kujiepusha na utaratibu wa matumizi ya mawakala katika manunuzi ya Umma, Sheria ya manunuzi (PPRA) ipewe meno zaidi na ifanye kazi kwa kujitegemea bila kusimamiwa na Wizara ya Fedha.
Kamati hiyo pia ilipendekeza serikali kupitia upya mikataba yote na kuweka kumbukumbu ya mikataba hiyo katika ofisi za bunge, timu ya Serikali inayoshauri mikataba (GNT) iwajibishwe, aliyekuwa waziri wa nishati na Madini, Nazir Karamagi na Mwanasheria Mkuu wa Serikali wawajibishwe.
Wakati huo huo, wabunge sita wanatarajia kutoa hoja binafsi zitakazojadiliwa katika kikao cha bunge hilo.
Siku za hivi karibuni Wabunge wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania wameonekana kuwa mwiba kwa serikali ambapo wamekuwa wakihoji bila woga utendaji wake kwa maslahi ya wananchi.
Wabunge hao kila mmoja tayari wamepeleka hoja binafsi katika maeneo tofauti huku wengi wao wakihoji moja kwa moja utendaji wa serikali na matumizi mabaya za umma.
Wabunge waliopeleka hoja binafsi ni Raphael Chegeni (Busega), William Shellukindo (Bumbuli), Alloyce Kimaro (Vunjo), Godfrey Zambi (Mbozi Mashariki), wote wa CCM na mmoja kutoka Chadema, Said Arfi (Chadema).
Source: Mwananchi, 5/4/2008
Posted by
Godfrey
at
19:50
0
maoni/comments
Muswada wa umeme wapigwa danadana
HATIMA ya kupelekwa bungeni kwa muswada wa sheria mpya ya umeme, imezidi kuchukua sura mpya baada ya Kamati ya Nishati na Madini kushindwa kutoa msimamo wake na kuahidi kuutoa Ijumaa ijayo mjini Dodoma wakati wa vikao vya Bunge.
Uamuzi huo ulitangazwa jana na Kaimu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Daniel Nswanzugwanko, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu umamuzi wa kamati hiyo.
Alisema muswada huo ulikuwa moto zaidi kutokana na baadhi ya wabunge kutokubaliana nao kutokana na kuonekana una lengo la kuliua Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) na kuzipendelea zaidi kampuni zitakazokuja kuwekeza katika sekta ya umeme.
Alisema Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, aliwasilisha baadhi ya mabadiliko yaliyoshauriwa na baadhi ya wabunge katika semina ya kujadili muswada huo wiki iliyopita, ambapo kwa kiasi kikubwa amejibu na kurekebisha matatizo yaliyoonekana.
Alisema kamati imemuamuru Waziri Ngeleja kwenda kuyaandika vizuri zaidi majibu yake na ayawasilishe katika kikao kijacho ambacho kitafanyika mjini Dodoma.
“Haya masuala ni nyeti sana na tunahitaji kujipanga vizuri ili tuweze kwenda mbele zaidi na pia kuepukana na masuala yaliyotokea katika mkataba wa Richmond,” alisema Nsanzugwanko.
Aidha, alikanusha tuhuma zilizoenezwa na baadhi ya watu kuwa kamati yake imerubuniwa na serikali, ili ipitishe muswada huo ambao ulizua utata mkubwa miongoni mwa wabunge wiki iliyopita.
Alisema kamwe kamati yake haiwezi kurubuniwa kwani kila mbunge ana kiu ya kuwa na umeme katika jimbo lake, ili uweze kuharakisha maendeleo na kutokomeza umasikini miongoni mwa jamii.
Awali, baada ya kutokubalika kwa muswada huo na wabunge katika semina iliyoandaliwa, Ngeleja na Naibu wake, Adam Malima, walilazimika kutumia nguvu nyingi kuwashawishi wabunge ambao walionekana kutoelewa somo.
Source: Tanzania Daima, 05/4/2008
Posted by
Godfrey
at
19:46
0
maoni/comments